KIJANA: "KWA NINI NIOTE NAFANYA MAPENZI"

Tuesday, July 100 comments



Karibu tena ndugu mpendwa katika blog yako uipendayo. leo napenda tujadiliane jambo hili ambalo limekuwa likiwatatiza wengi wetu katika jamii. Ni kwa nini watu wengi hususani vijana wanajikuta wakiota wanafanya mapenzi usingizini.
 Miongoni wa makundi ya vijana hasa wenye umri wa kati miaka 15-23 wengi wao huota wakifanya mapenzi ndotoni, lakini mbali na hao kuna watu wazima pia ambao hukumbwa na tukio hili. Uotaji wa ndoto hii umekuwa ukitafsiriwa na wengi kwa maana tofauti tofauti, huku wengine wakiuhusisha na ufanyaji mapenzi na Majini.

Uchunguzi unaonyesha kuwa uotaji ndoto za kimapenzi huwatokea hata watu ambao hawajawahi kufanya kitendo hicho kabisa, huku watu wanaofanya nao wakiwa ni wale wanaowafahamu kwa sura au wasiowafahamu. Wengi wamekuwa wakijiuliza maswali mengi juu ya nini kinachangia uotaji huu wa ndoto za kimapenzi?

Kitaalamu ndoto hizi hutokana na mawazo ya mtu husika ambayo yanaweza kugawanywa katika sehemu mbili ambazo ni MAWAZO YALIYO WAZI au YALIYOJIFICHA. Mtaalamu wa masuala ya ndoto Daktari Gillian Holloway anaeleza kuwa  ndoto hizi hufumbua maamuzi na hisia zilizojificha  nyuma ya ubongo.

Pamoja na tendo hili kuwa baya katika mitazamo ya wengi hasa ya kiimani, lakini bado si kitaalamu halina ubaya kwa kiwango hicho kwani mara nyengine husaidia kutafsiri yale ambayo wahusika hawakupata kuyafahamu kabla. Kwa mfano vijana ambao hawajafanya mapenzi hupata kutambua raha itokanayo na kitendo hicho na hivyo kuwaamshia hisia za kimapenzi ambazo pengine hawakuwa nazo hapo awali.

Wachunguzi wengi wa masuala haya ya ndoto wanasema, ndoto aina hizi zikitumika vizuri zinaweza kumsaidia mtu kumpata mchumba anayegusa hisia za moyo wake, aina ya mapenzi yanayomfurahisha, haiba ya mpenzi umpendaye na wakati mwingine huchangia kuongeza uzalishaji wa homoni na kupunguza msongo wa mawazo sawa na mtu aliyefanya mapenzi laivu.

Kwa maana hiyo watu wanaotajwa kutokewa na kitendo hicho mara kwa mara ni wale wenye tabia ya kuogopa wanaume/wanawake na hivyo kuzikandamiza hisia zao, wanaochochea hamasa za kingono na kutokuzikata, (mfano wanaochezeana tu na kuachana bila kufanya ngono), wanaotazama picha za ngono, wanaozungumzia sana mambo ya kimapenzi na wale wanaowaza sana wapenzi wao walio mbali.

Kwa maana hiyo ili mtu asiweze kutokewa na ndoto hizo hana budi kujizuia na mambo hayo yanayotokana na uamshaji na ukandamizaji wa hisia za kingono. Hii ina maana ya utashi wa mtu wa kutopenda kuota, lakini si kwamantiki kuwa uotaji huu unauhusiano na mambo ya kishirikina au kichawi kama ambavyo watu wengine wanavyoaminishwa.

Mwisho kama kuna wanaodhani kuwa ndoto hizi zimewadhuru kwa namna moja au nyingine, wafahamu kuwa kilichowadhuru si kuota ndoto hizo bali ni wasiwasi wao unaotokana na kusikia na wala si madhara kwa maana ya kuota kwenyewe, kwani ikiwa ni ndoto hata wanyama kama Mbwa, Paka na Sungura nao huota wakifanya mapenzi, ushahidi ambao unatosha kutupilia mbali hoja ya ndoto kutokana na majini.

Weka Comments zako kuhusu ya hili!!
Share this article:

Unaonaje huu Muonekano?

 
Support : Management

Copyright © 2011. Al-amini Official blog - All Rights Reserved
Template Modify by Al-Amini
Proudly powered by Blogger