Wanawake wanaongoza Kurudi Nyumbani na Mifuko yenye chochote

Wednesday, September 250 comments

Katika jamii ni kweli kwamba wanawake ndio watu wanaoijali sana familia kuliko wanaume, na ndipo pia inapojitokeza tofauti kati ya mwanaume na mwanamke katika suala zima la kujali familia kwa mtazamo wote, ikiwemo mapenzi katika familia. Kwa mujibu na Utafiti Uliofanyika katika meza yetu, Wanawake Ndio wanaongoza Kurudi Nyumabani na Mifuko yenye zawadi kwa ajili ya familia zao.

Utafiti umeonesha kuwa, katika kila wanawake kumi wanaokwenda kazini asubuhi, saba wanaporudi nyumbani jioni huwa wemebeba mifuko yenye vitu kama chakula, “viguo” na zawadi nyenginezo kwa ajili ya watoto na wapenziwao.
Utafiti wa kina uliofanya na Meza yetu hii umebaini kuwa kati ya jinsia mbili zilizopo duniani, wanawake ndiyo wanaongoza kwa kukumbuka familia na kuamua kuwabebea chochote kuliko wanaume.

Wakati Utafiti kwa wanawake umeona hilo, wanaume wao, katika kila kumi wanaokwenda kazini asubuhi, watatu tu ndiyo wanweza kukumbuka kubeba chochote kwa ajili ya familia.

Saba waliobaki, mara nyingi hushindwa kubeba chochote kwa sababu baada ya kutoka kazini huanzia Baa kabla ya kurejea nyumbani na wakiwa baa vitu wanavyonunua ni vile vinavyowahusu, na wakirudi nyumbani labda wamenunua vitu kwa ajili yao binafsi kama viatu, mashati, tai n.k

                                   TOA MAONI YAKO JUU YA HILI
Share this article:

Unaonaje huu Muonekano?

 
Support : Management

Copyright © 2011. Al-amini Official blog - All Rights Reserved
Template Modify by Al-Amini
Proudly powered by Blogger